Tuesday, September 19, 2017
NGO'MBE 345 WAPIGWA MNADA MEATU
Na Berensichina,sept
17,2017,ngombe 345 wapigwa mnada,
hakimu mkazi
mwandamizi mfawidhi wa mahakama ya mkoa wa simiyu john nkwabi ameamuru
kutaifishwa na kipigwa mnada jumla ya
ngombe 345 waliokamatwa wakichunga katika pori la akiba la maswa kinyume
cha sheria ya wanyamapori
akizungumza
mara baada ya kumalizika kwa mnada huo uliofanyika wilayani meatu meneja wa
pori la akiba la maswa lusato masinde amesema wameamua kuuza mifugo hiyo baada
ya mahakama kutoa amri kulingana na
sheria ya wanyama pori namba 5,2009 kifungu cha 111.
aidha meneja
huyo amewaonya wafugaji ambao watakaidi agizo la mhe.rais la kuondoa mifugo yao
kwa hiyari na kuacha kuchungia katika pori hilo
kwani msako wa kukamata mifugo hiyo ni endelevu na mifugo itakayokamatwa
itaendelea kutaifishwa kwa mjibu wa sheria
kwa upande
wake darali aliyesimamia zoezi la kuuza ngo’mbe hao kutoka kampuni ya abajaja
christopher kabenga amewataka wanunuzi wote kuhakikisha wanatembea na
stakabadhi halisi waliyopewa wakati watakapo kuwa wanasafirisha mifugo hiyo ili
kuepuka usumbufu njianii
RPC MARA AHIDI USHIRIKIANO NA ASKARI WA SERENGETI
na Berensichina,bunda,sept20,2017,Rpc
Mara ahidi ushirikiano na askari wa hifadhi ya Serengeti.
kamanda wa
polisi mkoa wa mara kamishina msaidizi wa polisi jafari mohamed amesema jeshi
la polisi mkoani mara litahakikisha linashilikiana na askari wa hifadhi ya
taifa ya serengeti katika kuhakikisha wanakomesha vitengo vya ujangili katika
hifadhi hiyo,
kamanda
jafari ameyasema hayo mara baada ya kumalizika kwa kikao kazi kilichofanyika
wilayani bunda ambacho kimewahusha wahifadhi toka hifadhi ya taifa ya serengeti
waendesha mashitaka wakuu wavitengo vya
ulinzi wa wanyamapori na ofisi ya mwandesha mashitaka mkoa wa mara lengo likiwa
ni kuweka mkakati namna ya kupambana na ujangili,
akizungumza
kwa niaba ya wahifadhi wa hifadhi hiyo,mhifadhi emanuel matungwa amesema
changamoto ya ujangili katika hifadhi hiyo ni kubwa kwani kila kukicha
majangili wanabuni mbinu mpya hivyo jitihada za pamoja zinahitajika katika
kupambana na vitendo hivyo,
kwa upande
wake wakili wa serikali mwandamizi toka
wa mkoani mara anisus kahindura,amesema ofisi yake imejipanga ili
kuhakikisha kesi za nyara zinamalizika mapema ili kuondoa msongamano wa kesi
hizo mahakamani
Saturday, August 5, 2017
VIDEO: wavamia msafara wa rais Magufuli, wakitaka aongee nao
Mwishoni mwa wiki hii, rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli, akishirikiana na mwenzake wa Uganda, Yoweri Museveni, walizindua ujenzi wa bomba la mafuta ghafi, litakalojengwa kutokea Hoima nchini Uganda hadi kijiji cha Chongoleani, mkoani Tanga.
Hata hivyo, akiwa njiani kuelekea Tanga kuhudhuria tukio hilo kubwa, rais Magufuli, alilazimika kusimama njiani baada ya wananchi kuusimamisha msafara wake, wakitaka aongee nao, jambo ambalo alilitekeleza, kama inavyoonekana katika video hii
MAGUFULIA NA MUSEVENI WAWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UJENZI WA BOMBA LA MAFUTA KUTOKA HOIMA HADI TANGA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake, Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakivuta utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi la mradi mkubwa wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Tanga huku viongozi mbalimbali wa Tanzania na Uganda wakishuhudia. Shughuli hiyo ilifanyika katika kijiji cha Chongoleani nje kidogo ya jiji la Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mkono wa pongezi na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la mradi mkubwa wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Tanga huku Viongozi mbalimbali wa Tanzania na Uganda wakishuhudia. Shughuli hiyo ilifanyika katika kijiji cha Chongoleani nje kidogo ya jiji la Tanga
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari mbalimbali waliohudhuria shughuli ya uwekaji wa jiwe la msingi la mradi mkubwa wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Tanga katika kijiji cha Chongoleani nje kidogo ya jiji la Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Chongoleani kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la Msingi mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka nchini Uganda hadi Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni katika uwanja wa ndege wa Tanga mara baada ya kuweka jiwe la msingi mradi mkubwa wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Tanga katika kijiji cha Chongoleani nje kidogo ya jiji la Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono pamoja na mke wake Mama Janeth Magufuli, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati wakiagana na Rais wa Uganda Yoweri Museveni katika uwanja wa ndege wa Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akicheza ngoma ya msanja na Mama Janeth Magufuli pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan mara baada ya kumsindikiza Rais wa Uganda Yoweri Museveni katika uwanja wa ndege wa Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia katika viwanja vya Chongoleani kabla ya tukio la uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakati wakielekea kuweka jiwe hilo la msingi.
Wasanii wakitumbuiza katika uwanja wa Chongoleani.
Wananchi mbalimbali waliohudhuria katika sherehe hizo za uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa bomba la mafuta
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakiwa katika picha ya pamoja na wasanii mbalimbali mara baada ya kutumbuiza.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni akihutubia katika viwanja vya Chongoleani nje kidogo ya jiji la Tanga. PICHA NA IKULUThursday, August 3, 2017
Matukio wakati wa RSA Day 2017, mjini Dodoma
Hivi karibuni, Mtandao wa Mabalozi wa Usalama Barabarani (RSA Tanzania), uliadhimisha siku ya mabalozi wa usalama barabarani mwaka 2017, ambapo katika maadhimisho hayo, mbali ya uelimishaji wa abiria katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani tokea mjini Dodoma, maandamano na hotuba mbalimbali, pia michezo na burudani mbalimbali zilipamba maadhimisho hayo, kama inavyoonekana katika video zifuatazo.
Mmoja wa mabalozi wa Usalama Barabarani,ambaye pia ni msanii, akitumbuiza wakati wa maadhimisho hayo
Mbali ya shughuli za uelimishaji, siku hiyo ilihitimishwa na michezo kadhaa, ukiwemo huu wa kukimbiza kuku.
IGP Sirro, atembelea Ubungo kujionea huduma za usafirishaji
Hivi karibuni, Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro, alitembelea kituo cha mabasi yaendayo mikoani kutokea jijini Dar es Salaam, Ubungo kwa ajili ya kujionea namna gani huduma za usafirishaji wa abiria zinaendeshwa kituoni hapo.
Hapa ni alichokisema IGP Sirro, baada ya ziara hiyo ambayo ilivuta hisia za abiria wengi waliokuwa kituoni hapo siku hiyo ya tukio
Hapa ni alichokisema IGP Sirro, baada ya ziara hiyo ambayo ilivuta hisia za abiria wengi waliokuwa kituoni hapo siku hiyo ya tukio
Watoa huduma katika hifadhi ya Serengeti
Miongoni mwa mamvo yanayoifanya hifadhi ya Serengeti, kuwa ya kwanza kuiwaza unapofikiri mahali pa kwenda kutalii, ni pamoja na watoa huduma mbalimbali, ambao wamesheheni vifaa na ukaribu wa kutosha.
Blogi hii, ilipata fursa ya kutembelea hifadhini humo hivi karibuni na kushuhudia baadhi ya wageni waliokuwa wametembelea mahali hapo wakiwa wanafurahia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na huduma za uhakika ambazo walizipata kutoka kwa makampuni ya usafiri yenye kutoa huduma za usafiri ndani ya hifadhi hiyo.
Watoa huduma hususan za usafiri ndani ya hifadhi ni wenye magari ambayo yanakidhi mahitaji ya hali zote za hewa katika mwaka mzima, pamoja na hali ya barabara zote katika eneo la hifadhi
Blogi hii, ilipata fursa ya kutembelea hifadhini humo hivi karibuni na kushuhudia baadhi ya wageni waliokuwa wametembelea mahali hapo wakiwa wanafurahia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na huduma za uhakika ambazo walizipata kutoka kwa makampuni ya usafiri yenye kutoa huduma za usafiri ndani ya hifadhi hiyo.
Watoa huduma hususan za usafiri ndani ya hifadhi ni wenye magari ambayo yanakidhi mahitaji ya hali zote za hewa katika mwaka mzima, pamoja na hali ya barabara zote katika eneo la hifadhi
Miongoni mwa watia huduma za usafiri waliobobea katika shughuli hiyo, ni pamoja na kampuni ya Zara Tanzania Adventures, kama magari yao yanavyoonekana pichani. Ni yenye ubora wa hali ya juu
Wengine ni kampuni ya Altezsa, ambao nao wana magari ya uhakika miongoni mwayo yakiwa haya yenye kuonekana katika picha hizi hapa juu
Serengeti National Park, hifadhi yenye utajiri wa vivutio
Hifadhi ya Serengeti, ni miongoni mwa sehemu chache sana nchini, na pengine hata duniani, ambazo zimejaaliwa kuwa na karibu kila kitu anachoweza kuhitaji mwanadamu, ili kumfanya afurahie uwepo wake mahali hapo.
Hapa, ni mkusanyiko wa baadhi tu, ya vitu ambavyo kwa hakika vitakufanya usijutie uamuzi wako wa kutembelea hifadhi hii, iliyosheheni mambo mengi ya kujifunza.
Hapa, ni mkusanyiko wa baadhi tu, ya vitu ambavyo kwa hakika vitakufanya usijutie uamuzi wako wa kutembelea hifadhi hii, iliyosheheni mambo mengi ya kujifunza.
Sunday, July 30, 2017
Ukataji miti wazidi kushamiri pori la Maswa
Vitendo vinavyoweza kutafsiriwa kama ni kuhujumu ustawi wa misitu muhimu kwa ustawi wa sekta ya utalii nchini, vimeendelea kukithiri hususan ukataji miti, ambao umekuwa ukifanywa na watu mbalimbali katika misitu mbalimbali nchini, likiwemo pori tengefu la Maswa.
Hivi karibuni, kamera ya Serengeti Wildilife & Nature Conversation, ilitembelea pori hilo, na kushuhudia miti iliyokatwa na wananchi hao wasio na nia njema kama picha zinavyoonekana.
Baadhi ya miti iliyokutwa imekatwa wakati wa ziara hiyo fupi ya kikazi.
Askari wa pori hilo, ambao wameelezea kusikitishwa na vitendo vua ukataji huo wa miti ambavyo vimekuwa vikifanywa kwa ujanja mkubwa katika kuwakwepa askari wanaolinda pori hilo
Subscribe to:
Comments (Atom)
Comments System
disqus
Disqus Shortname
msora
Popular Posts
-
SABABU RASMI ZA MGAWANYIKO WA WENGE MUSICA BCBG 4X4 TOUT TERRAIN NA MIAKA MITATU YA MWANZO YA BCBG NA MAISON MERRE – (Sehemu...
-
Huha Makuja Nyungi (kushoto), akiwa anaelekea mahakamani muda mfupi kabla ya kusomewa hukumu hiyo. Kulia ni mtuhumiwa mwingine katika ke...
-
Mwezeshaji wa mada ya kwanza kuhusu umuhimu wa TIKA, ndugu Derick Ndetabula akitoa mada kwa washirik.
-
! Tembelea sehemu maalumu kuhusu maisha ya walemavu wa ngozi Afrika Mashariki na juhudi za kuwalinda.
Header Ads


































